Majibu ya Spika Ndugai kwa wanaokosa utaratibu wa Bunge kuwasilisha ripoti zake serikalini



Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amewajibu watu wanaokosoa utaratibu wa ripoti za kamati za bunge kuwasilishwa serikalini kabla ya kufikishwa bungeni kama ilivyozoeleka, na kuwataka wananchi kuwapuuza watu hao kwa kuwa hawana nia njema.

Akizungumza katika sherehe ya  Makabidhiano ya taarifa za kamati maalum za kuchunguza uvuvi wa bahari kuu na gesi asilia, Spika Ndugai amesema utaratibu huo ni mzuri kwa kuwa unaweka mkazo katika utekelezaji wa ripoti hizo.

Spika Ndugai ameeleza kuwa “Sisi tumeanzisha utaratibu huu ambako tunafanya kazi yetu tunakuja mbele ya umma tunawasilisha kazi yetu mbele ya serikali yetu, eti tunaambiwa sisi tuna utaratibu mbaya, tuwapuuze watu wa namna hii sababu hawana nia njema.”

“Ningependa kufafanua kitu kidogo, ziko namna mbalimbali ya bunge kufanya kazi moja wapo ya ile tuliyoizoea ambapo bunge linafanya kazi ndani ya ukumbi wa bunge, namna nyingine ndiyo hii ambapo spika akishauriwa na kuona jambo hili lina msingi mkubwa anatumia mamlaka aliyonayo kufanya hivi nilivyofanya. Na kwa mamlaka hayo hayo akaamua kuwasilisha ripoti ile kwa serikali kwa utaratibu atakaona unafaa na utaratibu nilioona unafaa ni huu,” amefafanua Spika Ndugai na kuongeza.

“ Wako watu ambao wamekuwa wanakosoa huu utaratibu, na kama nilivyosema utaratibu huu ni mzuri toka uhuru tumekuwa na uongozi mbalimbali katika bunge, kamati za namna hii sio kwamba zilikuwa haziundwi zilikuwa zinaundwa, lakini ilikuwa spika akipokea taarifa ile anachofanya anaandika covering letter anaipeleka kwa serikali, serikali inaweka katika droo, mambo yote yameisha kila kitu kinaendelea kama kawaida.” 

Post a Comment

Previous Post Next Post