Ngorongoro Heroes yajinoa vikali kuikabili Mali


Timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 20 nchini (Ngorongoro Heroes) itacheza na timu ya Taifa ya Mali kwa vijana chini ya Umri wa miaka 20 Jumapili Mei 13,2018 Uwanja wa Taifa jijini  Dar es Salaam.
  
Kwa sasa Ngorongoro Heroes wapo kambini wakiendelea kujifua na mchezo huo, ili kuwakabili vyema vijana wa mali na kesho  watafanya vipindi viwili  vya mazoezi yaani asubuhi na jioni .

Taarifa za ndani kutoka kwa mkufunzi mkuu wa Timu hiyo Ammy Ninje,amethibitisha kumuacha mlinda mlango nambari moja wa timu hiyo Ramadhani kabwili,ambae ameondoka  kuelekea Algria na klabu yake ya yanga kuvaana vikali na USM Alger katika kombe za shirikisho barani Afrika

Kikosi hicho hakina majeruhi vijana wana morali kubwa ya kufanya vizuri katika mchezo huo wa kwanza wa raundi ya pili ya kufuzu fainali za vijana Africa.

Mchezo huo utachezwa majira ya saa 10 jioni na kiingilio katika mchezo huo  ni shilingi  elfu tatu (3,000)  kwa VIP  na kwa viti vya Mzunguko ni shilingi elfu moja (1,000).

Post a Comment

Previous Post Next Post