Serikali yapoteza zaidi ya Tril. 5 katika sekta ya uvuvi


Serikali imepoteza kiasi cha Sh. Trilioni 5.98 katika kipindi cha mwaka 2009 hadi 2017, pamoja na kupata hasara ya trilioni 3.169 kwa sababu ya mfumo mbovu katika sekta ya bahari kuu.

Hayo yamebainishwa leo na Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya Bunge ya Ushauri wa Uvuvi wa Bahari Kuu, Anastazia Wambura wakati akizungumza katika Makabidhiano ya taarifa za kamati maalumkuchunguza uvuvi wa bahari kuu na gesi asilia.

Vile vile, Wambura amesema serikali imekuwa ikipoteza bilioni 352 kila mwaka kupitia biashara ya usafirishaji samaki ghafi nje ya nchi.

Amesema hasara hizo zimetokana na changamoto zilizopo katika sekta ya uvuvi hali inayopelekea sekta hiyo kutotoa mchango mkubwa katika ukuzaji wa uchumi wa nchi.

  

Post a Comment

Previous Post Next Post