Polepole awavaa Zitto, Mbowe


Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Humphrey Polepole ameonyesha kushangazwa kwake na uamuzi wa Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe wa kutangaza ushirikiano wa vyama hivyo katika usimamishaji mgombea kwenye jimbo la Buyungu.

Jimbo la Buyungu lililoko mkoani Kigoma, liko wazi baada ya aliyekuwa mbunge wake, Marehemu Kasuku Bilkago kufariki dunia siku kadhaa zilizopita.


Polepole ameeleza kuwa, hatua hiyo aliyoiita ya kugawana ubunge imekiuka utamaduni wa kiafrika, na kwamba ilitakiwa wasubiri msiba wa marehemu Bilago uishe ndipo watangaze hatua hiyo.  


“Nimesikia jamaa palepale msibani walianza kugawana ubunge na kuanza kujihadaa, ni bahati mbaya sana. Utamaduni wa kiafrika ni kumaliza msiba ambapo lengo ni kufariji wafiwa. Nimekaa Kakonko kwa muda wa kutosha, kwakuwa mmeanza siasa msibani, CCM tunasema wembe ni uleule" amesema Polepole.

Post a Comment

Previous Post Next Post