Bunge laagiza vigogo BoT wahojiwe na PAC


Bunge limeagiza Bodi ya Benki Kuu ya Tanzania-BoT na manejimenti yake kufika mbele ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali-PAC kwa ajili ya kujieleza kuhusu matumizi ya bima binafsi ya matibabu.

Agizo hilo lilitolewa jana bungeni jijini Dodoma, na Spika wa Bunge, Job Ndugai ambapo alitoa muda wa wiki moja kwa bodi hiyo kufika mbele ya kamati ya PAC.

Spika Ndugai alitoa agizo hilo baada ya Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga kudai kwamba BoT kuna ufisadi wa watumishi wake kuendelea kutibiwa nje ya nchi.

Spika Ndugai aliagiza BoT, Mlinga na NHIF wakae kabla ya siku ya Jumatatu.


Chanzo: Mwananchi 

Post a Comment

Previous Post Next Post