Nchi ya Burundi inatarajia kuitambulisha Katiba mpya siku ya
Alhamisi, ambapo taarifa ya Ikulu imethibitisha kwamba sherehe za utiaji sahihi
kwenye katiba hiyo zitafanyika katika mkoa wa Gitega.
Aidhaa taarifa hiyo ya Ikulu imetoa mwaliko kwa magavana wote na
Wakuu wa tarafa za Burundi kushiriki kwenye sherehe hizo. Wamealikwa pia
wawakilishi wa vyama vya kisiasa , asasi za kiraia pamoja na Viongozi wa kidini
.
Itakuwa mara ya kwanza katika historia ya Burundi
kuwa na sherehe za kuipokea katiba mpya. Wadadisi wa siasa za Burundi wanahisi
utaratibu huo mpya ni ujumbe wa Rais Pierre Nkurunziza wa azama yake ya
kukamilisha shughuli ya katiba ambayo yeye ameipigia debe kwamba inakuja kuipa
Burundi hadhi na Uhuru wake kamili wa kujitawala .
Vile vile, Wajumbe wa Muungano wa
Ulaya wamelichagiza Shirika la Muungano wa Afrika kuchukua mikononi mazungumzo
ya amani ya Burundi kwa madai kwamba Jumuiya ya kimataifa imeanza kupoteza
imani kwa mchakato wa upatanishi unaosimamiwa na Jumuiya ya Afrika ya mashjariki
na inayoongozwa na Rais Museveni pamoja na msuluhishi Benjamin Mkapa.
Chanzo: BBC Swahili
