Vigogo walioshtakiwa Kenya kwa ufisadi kusota rumande wiki moja


Mahakama nchini Kenya imeamuru vigogo 24 walioshtakiwa nchini humo kwa kosa la ufisadi na kula rushwa, wakae rumande kwa muda wa wiki moja.

Watuhumiwa hao ni watumishi wa Shirika la Vijana wa Huduma kwa Taifa Kenya-NYS akiwemo Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Richard Ndubai na  Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana na Jinsia, Lilian Mbogo Omollo.

Mahakama imeamuru watuhumiwa hao wazuiliwe hadi siku ya Jumatano ijayo ambapo uamuzi wa kuachiliwa kwa dhamana utatolewa.
Walikamatwa na wengine wakajisalimisha kwa polisi Jumatatu wiki hii na kisha kufikishwa kortini Milimani, Nairobi jana. Kikao cha kusikizwa kwa kesi dhidi yao kiliendelea hadi usiku wa manane.

Chanzo: BBC Swahili

Post a Comment

Previous Post Next Post