Watanzania 11 walioshtakiwa Afrika Kusini kwa tuhuma za kubaka waachiwa huru


Watanzania 11 walioshtakiwa kwa kosa la ubakaji nchini Afrika Kusini wameachiwa huru na mahakama baada ya kukosekana kwa ushahidi.

Vijana hao mwaka jana walishtakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Johannesburg kwa makosa ya kumteka nyara na kumbaka mwanamke mjamzito ambaye ni raia wa Zimbabwe, Thelma Mondowa.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Johannesburg, Jaji Metisie aliwaachia huru.
Kisa hicho kilitokea mnamo 15 Mei mwaka 2015 katika barabara ya 270 Lilian Ngoyi mjini Johannesburg, ambapo mahakama hiyo iliarifuwa kwamba Mondowa alipata mkasa huo wakati akitoka kazini kwake na mfanyakazi mwenzake wa kiume ndipo wakavamiwa na kundi la wanaume wenye silaha ambapo, lakini mwenzie alifanikiwa kutoroka.
Wakili wa upande wa mashtaka wa serikali alikuwa amemfahamisha hakimu kuwa Bi Thelma Mondowa aliamua kurejea Zimbabwe na wameshindwa kupata anwani yake.
Chanzo: BBC Swahili




                                            

Post a Comment

Previous Post Next Post