Na. Aminah Kasheibar.
Staa wa muziki wa bongo fleva, Hamad Ally 'Madee' amesema
atashangaa kuona msanii anafanya tamasha Katika mwezi mtufuku wa Ramadhani.
Madee amesema kwasasa wapo katika mwezi mtukufu hivyo
inapaswa kusimamisha kazi zote za kimuziki na kufanya toba.
Alisema mwezi moja si miaka Mia ya kushindwa kufanya mema na
kutubu kwa mbele ya Mungu kwa yale tunayoyafanya.
"Mwezi huu tunapaswa kusimama na kuomba dua ili
tusamehewe kwa yale tuliyofanya ni jambo baya kuona msanii anafanya tamasha
Katika ramadhani.
"Hata kuimba haistiri lakini hatuna jinsi Ni moja ya
kazi ambayo inatupatia riziki ili familia zetu ziweze kupata mahitaji yao ya
kila siku," alisema Madee.
Hata hivyo Madee amesema anatamani hata mwezi mtukufu
usiishe kutokana na watu kuwa wastarabu na kuwa wanyenyekevu tofauti na miezi.
