Spika Ndugai amvunjia ukimya Mbowe kuhusu tuhuma za bunge kumtelekeza Bilago


Ikiwa imepita siku moja tangu Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe kulilalamikia bunge kwamba halikuwa mstari wa mbele katika kumuuguza aliyekuwa Mbunge wa Buyungu, marehemu Kasuku Bilago, Spika Job Ndugai amevunja ukimya kuhusu malalamiko hayo.

Spika Ndugai amemjibu Mbowe akisema kuwa, kama anataka uthibitisho kuhusu bunge lilivyojitolea kuhudumia matibabu ya marehemu Bilago, amuulize mke wa marehemu.

Amesema bunge lilimtunza marehemu Bilago na kumlipia gharama za matibabu tangu alipolazwa jijini Dodoma, pamoja na kukodisha ndege kwa ajili ya kumsafirisha kutoka Dodoma hadi Dar es Salaam na kumfikisha katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako umauti ulimfika wakati akipatiwa matibabu.   


“Mumtafute mke wake, ndio anaweza kuwaeleza kuhusu Bunge, ambao ndio tumemtunza tangu anaugua na kulipa gharama zote za matibabu, mpaka amefariki mikononi mwetu tukiwa tunamtunza mgonjwa, ukishafanya yote hayo halafu mtu aliyekuwepo  nje ya nchi, anasema kwamba wewe hakuna ulichokifanya, tuseme tu Haleluya Inatosha,” alisema Ndugai.

Post a Comment

Previous Post Next Post