Mugabe aligomea bunge, akacha kujibu tuhuma za ufisadi wa tril. 34


Rais mstaafu wa Zimbabwe, Robert Mugabe amegoma kuitikia wito wa bunge uliomtaka afike mbele ya kamati iliyoundwa kwa ajili ya kuchunguza mapato ya madini ya almasi nchini humo.

Kamati ya Nishati na Madini nchini humo, imetaarifu kuwa wito huo ulikuwa fursa ya mwisho kwa Mugabe kutoa utetezi wake mbele ya kamati hiyo kuhusu tuhuma hizo kwa kujibu maswali yake.

Kiongozi wa kamati hiyo, Themba Mliswa alisema walimwandikia barua ya wito Mugabe mara mbili, lakini hakuitikia wito huo.


Kamati hiyo imesema itatoa wito wa mwisho kwa Mugabe ili afike mbele ya kamati hiyo  Juni 11, 2018. 

Post a Comment

Previous Post Next Post