Matibabu ya Wema India yazua kizaa zaa mahakamani, atakiwa kuwasilisha nyaraka za uthibitisho


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemtaka msanii Wema Sepetu kuwasilisha mahakamani hapo nyaraka zinazothibitisha kupatiwa matibabu nchini India.

Uamuzi huo wa mahakama umekuja baada ya Wema kushindwa kufika mahakamani mara mbili mfululizo, ambapo imesema itatoa amri endapo mshtakiwa huyo atashindwa kuwasilisha nyaraka hizo.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba ndiye aliyetoa amri hiyo baada ya  mdhamini wa Wema ambaye ni mama yake mzazi, Mariam Sepetu kuwasilisha mahakamani hapo fomu ya matibabu.

Baada ya mdhamini huyo kuwasilisha fomu, zilipingwa na Wakili wa Serikali, Costatine Kalula kwa madai kuwa zilikuwa nyaraka za tiketi za ndege.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 13, 2018.

Post a Comment

Previous Post Next Post