Polisi nchini Kenya wanawashikilia maafisa watatu waandamizi
na Mkuu wa Shirika la Vijana wa Huduma kwa taifa-NYS, Richard Ndubai kwa tuhuma
za ufisadi.
Hatua hiyo imekuja baada ya agizo la Mwendesha Mashtaka Mkuu
wa Umma nchini humo, Nourdin Haji la
kuwataka watuhumiwa katika kashfa ya Sh. Bilioni 9 kushtakiwa.
Pia katika seke seke hilo, Washukiwa wengine kadhaa wamekamatwa
na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani katika kipindi cha saa 24, kulingana na
afisa mmoja katika ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma.
Pesa
hizo zinadaiwa kuchukuliwa kutoka kwenye shirika hilo katika kipindi cha miaka
mitatu, kwa mujibu wa duru mbali mbali.
Chanzo:
BBC Swahili
