Baada ya kung’atuka LHRC, Dkt. Kijo-Bisimba ahusishwa kuwa mjumbe Baraza la Wazee Chadema




Ikiwa zimepita siku mbili tangu Dkt. Hellen Kijo-Bisimba kustaafu nafasi ya Ukurugenzi Mkuu katika Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu-LHRC,yameibuka madai mitandaoni kwamba Bisimba ameteuliwa kuwa Mjumbe wa Baraza la Wazee la Chadema.

Taarifa hizo zilisambaa leo Mei 30, 2018 katika mitandao ya kijamii hasa wa WhatsApp kupitia barua iliyodaiwa kutolewa na Afisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene.


Mtandao huu ulimtafuta Makene kwa njia ya simu kwa ajili ya kuthibitisha taarifa hizo, ambapo amekanusha kwamba si za kweli. Barua hiyo inayodaiwa kuwa ni ya kughushi iko hapo chini. 


Post a Comment

Previous Post Next Post