Mchungaji atoa kali ya mwaka, waumini wamjia juu


Mhubiri anayefahamika kwa jina la Jesse Durplantis kutoka nchini Marekani amewaomba waumini wake wamnunulie ndege yake ya nne.

Durlantis amesema Mungu amemwambia anunue ndege aina ya Falcoln 7X inayogharimu dola milioni 54.
Mchungaji huyo amesema awali alikuwa na shaka kuhusu kuendelea na ununuzi huo, lakini Mungu alimwambia: "Sikukwambia uilipie. Nilikwambia uamini na utaipata."
Akikazia kuhusu dhamira yake hiyo, Durlantis amesema hata kama Yesu angekuwepo siku hizi, asingepanda punda kama ilivyokuwa zamani.

Hatua hiyo imeibua waumini wake na wadau wengine ambapo wamefananisha ombi hilo na ulafi wa mali.
Watu kwenye Twitter wamepokea ombi hilo kwa mshangao, wengi wakinukuu aya kwenye Biblia zinazotahadharisha dhidi ya ulafi na "manabii wa uongo".
Wengine wanasema pesa hizo zingetumika vyema kuwasaidia maskini.
Chanzo:BBC Swahili

                                              

1 Comments

Previous Post Next Post