Orodha ya wanamichezo tajiri duniani iliyotajwa na Forbes, yumo Ronaldo, Messi


Mwanamasumbwi wa Marekani Floyd Mayweather ametetea taji lake katika porodha ya Forbes ya wanamichezo wanaopata mapato ya juu zaidi duniani.
Alijipatia kipato cha $275m (£205m) katika mechi yake ua masumbwi mwezi Agosti dhidi ya nyota wa UFC star Conor McGregor, ambaye yuko nambari nne katika orodha ya jarida hilo la biashara nchini Marekani.
Cristiano Ronaldo ambaye alikuwa akiorodheshwa wa kwanza katika kipindi cha miaka 2 iliopita sasa ni wa tatu huku Lionel Messi akichukua wadhfa wa pili kwa tofauti ndogo.
La kushangaza ni kwamba hakuna wanawake katika orodha hiyo baada ya mwanamke wa pekee katika orodha hiyo Serena Williams kutoorodheshwa.
                                                                              
Wanamichezo 10 tajiri zaidi duniani.
1.       Floyd Mayweather - Ndondi ($285m)
2.       Lionel Messi - Kandanda ($111m)
3.       Cristiano Ronaldo -kandanda($108m)
4.       Conor McGregor - Karate, judo na Ndondi ($99m)
5.       Neymar - kandanda ($90m)
6.       LeBron James - Vikapu ($85,5m)
7.       Roger Federer - tenisi ($77.2m)
8.       Stephen Curry - Vikapu ($76.9m)
9.       Matt Ryan - Soka ya Marekani ($67.3m)
10.   Matthew Stafford - Soka ya Marekani ($59.5m)


Chanzo: BBC Swahili

Post a Comment

Previous Post Next Post