Bashe apata pigo, afiwa na mama yake mzazi


Mbunge wa Nzega, Hussein Bashe amepata pigo baada ya kuondokew na mama yake mzazi, Zainab Abdi.
Mama Bashe amefariki dunia leo katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyoko Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam.

Taarifa hizo amezithibitisha Bashe kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter.


“Ndugu zangu nimeondokewa na mama yangu mpendwa, Inna Lillahi wa inna ilayhi raji’un," ameandika Bashe katika ukurasa wake wa Twitter. 

Post a Comment

Previous Post Next Post