Chadema, familia ya marehemu Bilago yaligomea Bunge


Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe ameeleza kusikitishwa kwake na ratiba ya mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Buyungu, Kasuku Bilago iliyotolewa na Bunge siku mbili zilizopita, akisema kuwa maamuzi hayo hayakushirikisha chama hicho na familia ya marehemu.

Bunge kupitia ofisi ya katibu mkuu ilitoa ratiba ya mazishi ya marehemu Bilago, ambapo ilipanga mwili wake uagwe bungeni leo Jumatatu, lakini Mbowe amesema hatua hiyo imewahuzunisha sana kutokana kwamba imelenga kuharakisha mazishi ya Bilago.

“Bunge limeundwa na sehemu kuu mbili, serikali na kambi ya upinzani, katika kambi ya upinzani tuna vyama vingi, na upande wa serikali una ccm.bSisi tunaelewana sana lakini upande wa pili kuna urafiki wa mashaka na popote wanapojipa jukumu la kufanya maamuzi kuhusu upande wetu yamekuwa hayana nia njema,” amesema na kuongeza.

“Bilago alifariki jumamosi mchana, saa kumi jioni ofisi ya bunge imetangaza taratibu za mazishi wakati tuko katika harakati za kuhifadhi mwili, hatujakaa kikao, hatujawasiliana na ndugu, huyu ni kiongozi wa mikoa mitatu na mbunge. Pasipo mazungumzo ofisi inatoa taarifa ya mazishi hilo jambo limetuhuzunisha sana. Wamesema bilago aagwe leo kama wangekuwa wanampenda wamemtibu kwanza.”


Mbowe ameongeza kuwa “Wanataka kuharakisha kumzika kiongozi wetu, nikamwambia spika hatutokuja Dodoma Jumatatu. Ngoja tufanye mawasiliano na familia, familia ikasema Alhamisi ndiyo siku nzuri ya mazishi, sisi kama chama tulikubaliana na familia tukaiarifu ofisi ya bunge kwamba tutamlaza Alhamisi kijijini kwao, tukapanga ratiba asubuhi atapelekwa Dodoma kwa ajili ya wabunge wenzake kisha atapelekwa kigoma kwa ndege.”

Post a Comment

Previous Post Next Post