Kardinali Pengo atangaza kifo cha Paroko Msaidizi Parokia ya Mt. Yosefu


Paroko Msaidizi wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu katika Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Venance Tegete amefariki dunia jioni ya leo Mei 26, 2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili aliko lazwa kwa ajili ya matibabu kabla ya kufikwa na umauti.

Taarifa ya kifo cha marehemu Padre Tegete imethibitishwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.

Katibu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Pd. Frank Mtavangu amesema taratibu za mazishi zinafanywa na kwamba taarifa zaidi zitatolewa baadae.


Post a Comment

Previous Post Next Post