Mbunge wa Chadema afariki dunia, mwili wake kuagwa Bungeni Jumatatu


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amemlilia Mbunge wa jimbo la Buyungu (Chadema) kutoka mkoani Kigoma, Kasuku Samson Bilago aliyefariki dunia mchana wa leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kupitia taarifa yake aliyoitoa kwa umma leo Mei 26, 2018, Spika Ndugai amesema ofisi ya bunge inaendelea kuratibu taratibu za mazishi kwa kushiriukiana na familia ya marehemu Bilago.

Taarifa hiyo imeeleza kwamba mwili wa Bilago unatarajiwa kuagwa bungeni siku ya Jumatatu ya Mei 28, 2018 na baadae kupelekwa Kankonko mkoani Kigoma kwa ajili ya mazishi.


Awali marehemu Bilago alilazwa katika hospitali ya DCMC iliyoko jijini Dodoma ambapo baadae alihamishiwa Muhimbili alikofikwa na umauti.

Post a Comment

Previous Post Next Post