JKT yataja orodha ya wahitimu kidato cha sita waliochaguliwa kujiunga mafunzo ya jeshi


Jeshi la Kujenga Taifa-JKT imetaja orodha ya majina ya waliohitimu kidato cha sita walioteuliwa kujiunga na  mafunzo mbalimbali ikiwemo uzalendo, umoja wa kitaifa, stadi za kazi na maisha kwa ajili ya kulitumikia taifa.

Taarifa hiyo imetolewa leo kwa umma na JKT, ambapo imetaja tovuti yenye orodha kamili ya majina ya vijana walioteuliwa na makambi ya JKT waliyopangiwa, ambayo ni www.jkt.go.tz

Sehemu ya taarifa hiyo inaeleza kuwa, walioteuliwa watatakiwa kujigharamia nauli za kwenda na kurudi kwenye makambi ya JKT waliyopangiwa wakiwa na vifaa mbalimbali.


Vile vile JKT limewapangia kambi watu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho, ambayo imetajwa kuwa  Ruvu JKT iliyoko mkoani Pwani ambako ina miundombinu ya kuhudumia jamii hiyo.

Post a Comment

Previous Post Next Post