Korea Kaskazini yakubali kuondoa silaha za nyuklia, kukutana na Trump


Korea Kaskazini imekubali kuondoa silaha za nyuklia katika rasi ya Korea pamoja na kuhudhuria mkutano wa kukutana na Rais wa Marekani, Donald Trump unaotarajia kufanyika Juni 12, 2018 Singapore.  

Taarifa hiyo imethibitishwa na Rais wa Korea Kusini, Moon Jae-in baada ya kufanya kikao jana Jumamosi na Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un.

Mkutano huo kati ya viongozi wa Korea kaskazini na Korea Kusini ni mabadiliko ya hivi karibuni, katika wiki iliyogubikwa na misukosuko ya kidiplomasia kuhusiana na mkutano wa kilele wa aina yake ambao haukuwahi kutokea kati ya Marekani na Korea Kaskazini.


Chanzo: D.W Swahili

Post a Comment

Previous Post Next Post