Aliyeongoza kamati ya kuhakiki mali za CCM ateuliwa kumrithi Kinana


Mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Kuhakiki mali za CCM iliyoundwa na mwenyekiti wake  Rais John Magufuli, Dkt. Bashiru Ally ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho.

Dkt. Bashiru ambaye ni Mwalimu Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ameteuliwa na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM- NEC kuurithi wadhifa huo uliokuwa chini ya Abdulrahman Kinana kabla ya kujuzulu hivi karibuni.



Wajumbe wa NEC walimteua Dkt. Bashiru kuwa Katibu Mkuu wa CCM katika Mkutano wake uliofanyika leo kwenye Ukumbi wa Kikwete ulioko Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Post a Comment

Previous Post Next Post