CCM yamuachisha uanachama mwakilishi Zanzibar, yatoa onyo kwa wabunge wa EALA


Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi-CCM Taifa- NEC imemuachisha uanachama Mwakilishi wa Jimbo la Jang’ombe liliko visiwani Zanzibar, Abdallah Diwani, pamoja na kutoa karipio kwa wajumbe wa Bunge la Afrika Mashariki-EALA, Fancy Nkuhi na Mariam Ussi Yahya.

Adhabu hizo zimetolewa leo na Wajumbe wa NEC katika kikao chake kilichofanyika leo Mei 29, 2018 jijini Dar es Salaam baada ya wajumbe hao kuazimia kuwaadhibu makada hao wa CCM.

Sehemu ya taarifa iliyotolewa kwa umma na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole, inaeleza kuwa  Diwani ameachishwa uanachama kwa kosa la kwenda kinyume na miiko ya uongozi wa CCM.

Wakati Nkuhi na Mariam Yahya ambao ni wajumbe wa EALA wamepewa karipio kali kwa kosa la kuwa na mwenendo usioridhisha na kulinda maslahi ya nchi unaokinzana na misingi na miiko ya uongozi.

Wajumbe hao wa EALA wamewekwa chini ya uangalizi wa kimaadili kwa muda wa miezi kumi na nane.


Post a Comment

Previous Post Next Post