Ahadi ya Ngorongoro Heroes dhidi ya Mali


Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) Ammy Ninje ameahidi ushindi katika mchezo wao wa raundi ya pili kufuzu fainali za Afrika kwa Vijana dhidi ya Mali, mchezo  utakaochezwa Jumapili Mei 13, mwaka huu  kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Ninje amesema anafahamu vyema kuwa Mali ni timu nzuri na amekuwa akiifuatilia kwa karibu, lakini kwa upande wa Ngorongoro Heroes wao wamejiandaa vizuri  kuhakikisha wanafanya vema katika mchezo huo

Naye Nahodha wa Ngongoro Heroes, Issa Makamba  amesema kikosi chao kipo tayari kwa mapambano na  wanaamini watashinda.

Watanzania wanatakiwa kujitokezaa kwa wingi katika uwanja wa taifa, kuwashangilia Ngorongoro Heroes, mchezo utakaoanza majira ya saa 10 alasiri, kiingilio katika mchezo huo ni Sh. 3,000  kwa VIP na Sh. 1,000 kwa viti vya mzunguko.

Post a Comment

Previous Post Next Post