ACT yamlilia Bilago


Chama cha ACT-Wazalendo kimetoa salamu za pole kwa chama cha Chadema, bunge na familia ya aliyekuwa Mbunge wa Buyungu mkoani Kigoma, Kasuku Bilago aliyefariki jana katika hospitali ya taifa Muhimbili.

Salamu hizo zimetolewa leo Mei 27, 2018 na Katibu wa Itikadi na Uenezi ACT, Ado Shaibu wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Ado amesema ACT itashirikiana kwa karibu na familia ya marehemu ya Bilago katika kufanikisha shughuli za mazishi.

“ACT tunapenda kutoa pole kwa Chadema, bunge na wananchi wa Buyungu mkoani Kigoma kwa kuondokewa na mbunge wao mpendwa Kasuku Bilago, katika kipindi hiki kigumu tuko nao bega kwa bega,” amesema Ado.


Taarifa ya ofisi ya bunge iliyotolewa jana kwa umma, ilieleza kuwa mwili wa marehemu Bilego unatarajiwa kuagwa kesho bungeni jijini Dodoma kisha kusafirishwa Kankonko mkoani Kigoma kwa ajili ya mazishi.

Post a Comment

Previous Post Next Post