“Wasanii tusibaguane”- Steve Nyerere



Na Aminah Kasheiba, 24SevenUpdater

Msanii wa filamu za Bongo Movie, Steve Nyerere amesema wasanii wanatakiwa kuwa na ushirikiano katika vipindi vya dhiki na faraja ili waweze kufika mbali kisanaa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Steve ametolea mfano msiba wa Masogange na kusema kuwa wasanii walishirikiana kwa muda wote hivyo ushirikiano huo uendelee kwani hakuna anaejua kesho.

“Tunapaswa kushikamana kwa kipindi chote kwani ushirikiano ndio unasaidia hata kazi zetu za sanaa kufika mbali majungu na fitina hazina msingi wowote ule.

“Sote ni kitu kimoja hivyo tunatakiwa kushikana na kuwa mfano kwa jamii ukizingatia sisi ni kioo cha jamii,’’ amesema Steve.

Post a Comment

Previous Post Next Post