Diamond ‘kutikisa’ Kombe la Dunia




Na Aminah Kasheiba, 24SevenUpdater

Nyota wa muziki wa bongo fleva, Nassib Abdul ‘Diamond Platinum’ anatarajia kushiriki kwenye uzinduzi wa Kombe la Dunia nchini Urusi.

Kombe la Dunia linatarajiwa kuanza mwezi , Juni mwaka huu ambapo Diamond atakuwa Balozi akiwakilisha wasanii wengine kutoka Tanzania.

Baadhi ya wasanii wanaoungana na Diamond Plantinum katika uzinduzi huo ni Jason Deruro, Cassper Nyovest na waimbaji wengine kutoka nchi mbalimbali za Afrika kama Uganda, Ethiopia na Msumbiji ambao wataimba wimbo wa pamoja unaoitwa ‘Color’.

Diamond amesema amefurahi kupata fursa ya kushiriki kwenye uzinduzi huo na kuwa mmoja wa wasanii kutoka Tanzania.


Amesema kuwa nafasi aliyoipata atatuimia vizuri kwa lengo la kukuza soko la muziki wa Tanzania na kuitangaza nchi kupitia fursa hiyo.

“Nimefurahi kupata nafasi hii kwani inanipa nguvu ya kufanya kazi kwa bidii zaidi kwani fursa niliyoipata ni ya kipekee na nitaitumia vizuri.

“Wimbo wa ‘Color’ nitakaouimba kama remix ambao siku hiyo ndio nitaimba kwa lengo la kuitangaza tamaduni ya Tanzania ili watu wajue,’’ amesema Diamond.

Hata hivyo Diamond amesema wimbo huo wa ‘Color’ umeandaliwa na Emmanuel Mkono ‘Nahreel’.

Post a Comment

Previous Post Next Post