WARAKA wa wachungaji wa kanisa la kiinjili la kilutheri
Tanzania KKKT umeanza kupingwa kwa
hoja ya kuwa umeushambulia serikali
zaidi,
Philipo Mwakibinga Mkurugenzi wa Utafiti wa
Watetezi wa Rasilimali wasio na mipaka (Walami), akizungumza na vyombo
vya habari leo amesema kuwa waraka wa maaskofu hao umeelemea kuikosoa serikali
ambaopo wangeweza kuzungumzia masuala yao yahusiayo dini yao.
“Tunatoa wito kwa
Maaskofu wetu kujikita katika masuala mahsusi yanayohusu Dini, watuelimishe
kwenye dini, wamuachie Kaisari yaliyo yake
na Mungu yaliyo yake
“Tunashangaa ni
kwanini waraka huu wa salamu za Pasaka haukujikita zaidi katika kuwasisitiza waumini
wake kujikita katika kuabudu, kumnyenyekea Mungu, kusoma bibilia na maandiko
mengine ya dini na badala yake wakajikita katika maoni yanayong’ata na kupuliza”
amesema.
Msemaji huyo ameshangazwa na viongozi hao kuzungumzia suala
la katiba mya ilhali viongozi wa upinzani waliwahi kugoma kwenye bunge la
kujadili rasimu ya Katiba mpya.
“Sote ni mashahidi kuwa Kuilazimisha
Serikali kuitisha mchakato upya wa katiba ni jambo ambalo haliingii akilini kwa
sasa kutokana na ukweli kwamba ni wanasiasa wenyewe hususan wa vyama vya
upinzani ndio waliosusia na kukwamisha mchakato wa katiba kwa kutaka
kulazimisha mawazo yao yawe bila kuzingatia msingi mama wa Demokrasia kuwa
wachache wanasikilizwa wengi wanashinda” amesema.
Mwakibinga amesema kuwa anatilia shaka waraka huo kuwa
unamikino ya kisisasa kutoka madai ya kusambazwa na Mbunge wa Arusha Mjini
Godbless Lema.
“Kwanini waraka
huu wa Maaskofu umesambazwa kwa mara ya kwanza na kiongozi wa CHADEMA ambaye
pia ni mjumbe wa kamati kuu wa chama hicho mheshimiwa Lema ambaye ndiye aliusambaza Waraka wa Mbowe
katika muda unaofanana na njia zinazofanana”