Trump awatibua maswahiba zake, EU, Canada, Mexico Ujerumani waahidi kulipa kisasi


Hatua ya serikali ya Rais Donald Trump ya kuziwekea vikwazo vya kiushuru bidhaa za chuma cha pua na bati, imewatibua washirika wa Marekani ambapo Umoja wa Ulaya, Canada na Mexico zimeanza kulipa kisasi.

Mapema jana Juni mosi, 2018 Canada na Mexico zilitangaza hatua za kujibu ushuru mpya uliowekwa na Marekani dhidi ya bidhaa hizo zinazoingizwa nchini Marekani.

Wakati Canada na Mexico Zikitangaza uamuzi huo, Umoja wa Ulaya-EU unasema uko tayari kujibu hatua hiyo ya Marekani iliyochochewa na Rais Trump.

Ujerumani nayo haikuwa nyuma katika sakata hilo, ambapo inasema nayo itashirikiana na Canada na Mexico katika kuratibu mkakati wa pamoja dhidi ya Marekani. Uamuzi huo umetangazwa na Waziri wa Fedha wa Ujerumani, Peter Altmeier.

Nchi ya Ufaransa ambapo hivi karibu Rais wake, Emmanuel Macron alizungumza na Trump katika mazungumzo hayo alimuonya rais huyo wa Marekani kwamba amefanya makosa kuweka vikwazo hivyo na kwamba imefanya makosa.

Chanzo: D.W Swahili

Post a Comment

Previous Post Next Post