Maajabu: Mama akutana na mwanaye aliyejua amefariki miaka 30 iliyopita


Mama mmoja nchini Marekani amekutana na bintiye, Melissa Ohden aliyedhani kuwa amefariki dunia miaka 30 iliyopita kutokana na yeye kuitoa mimba yake.
Mnamo 1977, katika hospitali moja nchini Marekani katika jimbo la Iowa, Mamake Melissa aliyekuwa na umri wamiaka 19 alitoa mimba kwa kutumia kemikali kwa zaidi ya siku tano.
Melisaa alizaliwa akiwana miezi minane akiwa na kilo 1.3 na akatupwa kwenye taka taka za hospitali.Hapo ndipo nesi mmoja alisikia sauti ya mtoto akilia na kwa kuchungulia akaona mwili ukisogea.Melissa alikimbizwa katika chumba cha wagonjwa mahututi ambapo aliponea na kuishi.
Madaktari walidhani atakuwa hawezi kuona na kwa wakati mmoja walidhani ataugua matatizo ya moyo yasiotibika.Lakini amefanikiwa kusihi maisha yenye afya tele na amelelewana familia iliomuasili.
Melissa ambaye ameandika vitabu kuhadithia maisha yake anasema aligundua kwamba aliasiliwa wakati alipogombana na dadake kutoka familia iliomuasili.

Chanzo: BBC Swahili

Post a Comment

Previous Post Next Post