JamiiForums yaimwaga Serikali mahakamani



Mwanzilishi wa mtandao wa JamiiForums, Maxence Melo na mwenzake Micke William wameachiwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kukutwa hawana kesi ya kujibu katika Kesi namba 457 iliyokuwa ikiwakabili iliyofunguliwa na Jamhuri kuhusu kampuni ya CUSNA Investment iliyodaiwa kufoji nyaraka bandarini, kukwepa kodi na kuwatesa wafanyakazi wazalendo na kupendelea wageni toka nje ya nchi.

Akisoma shauri hilo Hakimu Godfrey Mwambapa amesema Washitakiwa hawana kesi ya kujibu na hiyo Mahakama imewaachia huru kuanzia leo.

Katika kesi hiyo, Polisi walitaka JamiiForums iwapatie taarifa za mwanzisha mada aliyefahamika kwa jina la Kwayu na mchangiaji mmoja Amri Shipuri ili waweze kuwakamata na kuwahoji kutokana na ukiukwaji wa taratibu.

 JamiiForums inadaiwa kuwa, ilikataa kutoa taarifa binafsi za mwanachama wake kwa kuamini kuwa chanzo hcho cha taarifa kilikuwa na nia njema hivyo kutaka kwanza iwepo Hati ya Mahakama inayoridhia kukamatwa kwa mhusika na kuelezwa kosa lake.

Kesi hiyo ni kati ya mashauri 3 yaliyokuwa yanawakabili washtakiwa, na kwamba kwa sasa bado kuna mashtaka 2 yanayowakabili washtakiwa hao, yatakayotajwa mahakamani hapo Juni 18 mwaka huu.



Post a Comment

Previous Post Next Post