Serikali kuwabana wakurugenzi wasiotoa fedha za wananchi


Serikali imesema itaingiza kipengele katika muswada wa fedha kitakachowalazimisha wakurugenzi wa halmashauri nchini kutenga na kutoa asilimia 10 ya mapato ya halmashauri hizo kwa ajili ya mikopo ya kina mama na vijana.

Hayo yamesemwa leo Bungeni jijini Dodoma katika kikao cha 43 mkutano wa 11 wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Anthony Mavunde wakati akijibu swali la Mbunge Viti Maalumu mkoani Mwanza, Kemirembe Lwota.

Kemirembe alihoji bungeni kuwa, serikali ina mpango gani katika kuziwezesha halmashauri kutoa fedha za mikopo kwa wananchi, ambapo alisema halmashauri nyingi nchini zimekuwa hazitoa fedha hizo.  


Waziri Mavunde amejibu kuwa “Kuna kipengele kitaingizwa kwenye muswada wa fedha ‘finance bill’ kitamlazimisha kila mkurugenzi hiki kiasi cha fedha kinatengwa na kinatolewa, sasa hivi ni option kutolewa, lakini kipengele hicho kikiingizwa  kisipotengwa watachukuliwa hatua za kisheria, tutaleta kipengele ili kuhakikisha fedha hizi zinatengwa.”

Post a Comment

Previous Post Next Post