Mahakama yaombwa kuunda tume kesi mauaji ya Bilionea Msuya


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeombwa kuunda tume kwa ajili ya uchunguzi kwenye kesi ya mauaji ya Bilionea Erasto Msuya.


Ombi hilo limewasilishwa leo Jumatatu  Juni 4, na Miriam Mrita Mtuhumiwa wa kesi hiyo ambaye alikuwa   Mke wa Marehemu Msuya  Mbele ya Thomas Simba, Hakumu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo.

Miriam na Mwengine  Revocatus  Muyela  wanatuhumiwa kwenye kesi namba 5 ya mwaka 2017 ambapo wanadaiwa  kuwa Tarehe 25 Mwezi Mei 2016 Maeneo ya Kibada , Kigamboni  jijini Dar es Salaam walimuwa  Aneth Msuya  dada wa marehemu Erasto Msuya.

Miriam  aliiomba Mahakama kuundwa kwa tume hiyo kutokana na madai yake kuwa kuna uonevu unaendelea kwenye kesi hiyo.

Ombi hilo amelitoa baada Patric Mwita  Wakili wa Serikali kuomba kuahalishwa kesi hiyo kwa madai kuwa jalada halisi la kesi hiyo lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).


Mwita ameiomba Mahakama kuihalisha kesi  na itajwe tarehe nyengine ndipo aliponyoosha mkono na hakimu akamruhusu aongee.


"Mimi ni mama mjane, mume wangu ameuawa, mimi nipo mahabusu gerezani kwa miaka miwili, kama mama sijui watoto wangu wanaendeĺeaje huko nje,”

“Alichagiza kuchelewaweshwa kwa upelelezi ambapo kila uchwao anaambiwa upelelezi haujakamilika. "Mtu ukishafiwa na mume kuna vurugu mechi zinaendelea huko nje, naomba iundwe tume ya uchunguzi wa kina ya kuichunguza kesi hii kwa sababu kuna uonevu ambao unaendelea,"Alieleza Miriam.



Post a Comment

Previous Post Next Post