Hans Pope aongezwa kwenye kesi ya Aveva na Kaburu


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imewaongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Pope na mkandarasi wa uwanja wa timu hiyo, Frank Peter Lauwo,  katika kesi ya utakatishaji fedha  inayowakabili Rais wa timu hiyo, Evans Aveva na makamu wake, Geofrey Nyange  'Kaburu'.

Mahakama hiyo imeagiza Hans Pope na Lauwo wafikishwe  mahakamani kujibu mashitaka hayo yanayowakabili ambapo amri hiyo imetolewa na Hakimu  Mkazi Mkuu Thomas Simba baada ya  washitakiwa hao kutafutwa bila mafanikio na  kuomba hati ya kuwakamata.

Kufuatia mabadiliko hayo washtakiwa  hao wamesomewa upya hati ya mashtaka na sasa wanakabiliwa  na  mashtaka 10 tofauti na hati ya awali iliyokuwa na mashtaka matano.

Kesi hiyo imahirishwa hadi Mei 14, 2018 kwa ajili ya kutajwa na kufuatilia kama washitakiwa hao wawili watakuwa wamekamatwa.

Post a Comment

Previous Post Next Post