Baada ya kukosa ubingwa, Mlinda mlango wa Liverpool abeba lawama, aomba radhi mashabiki



Mlinda mlango wa klabu ya Liverpool, Loris Karius amekubali kubeba lawama ya kukosa ubingwa wa Champion League baada ya timu yake kukubali kichapo cha mabao 3-1 dhidi ya mabingwa wa ligi hiyo Real Madrid.

Mlinda mlango huyo amekiri kwamba alifanya makosa makubwa mawili yaliyozaa magoli hayo katika mchezo wa fainali uliopigwa jana, na kuepelekea Real Madrid kutwaa ubingwa.

Makosa hayo ni pamoja na kuipa mwanya Real Madrid wa kupata bao la kuongoza katika dakika ya 51 kupitia mshambuliaji wake Karim Benzema. Karius alifanya kosa hilo alipojaribu kuharakisha kuanzisha mashambulizi ambapo alirusha mpira mbele ya Benzema.

Karius amewaomba msamaha mashabiki wa Liverpool kutokana na makosa hayo yaliyoigharimu klabu hiyo kukosa ubingwa.

"Naomba  samahani  kwa  kila  mtu, kwa  timu, kwa  klabu , kwamba makosa hayo  yameigharimu  timu. Iwapo  ningerudisha  nyuma muda , ningeweza. Nina  masikitiko  makubwa  kwa  timu  yangu. Nafahamu  nimewaangusha  leo. Magoli  haya  yametugharimu  kukosa  ushindi, kimsingi," alisema.



Post a Comment

Previous Post Next Post