Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless
Lema amesema kama ubaguzi wa rangi na vyama vya siasa nchini utaondoka kwa viongozi wa Chadema
kujiuzulu nyadhifa zao, wako tayari kufanya hivyo ili taifa libaki na
mshikamano.
Lema ametoa kauli hiyo leo Mei
30, 2018 katika shughuli ya kuuaga mwili wa aliyekuwa mbunge wa Buyungu mkoani
Kigoma, Marehemu Kasuku Bilago.
Lema amesema kuwa, undugu na
mshikamano katika taifa ni bora kuliko rangi na vyama vya siasa.
“Wabunge wa CCM wameondoka,
unajiuliza tunaishi katika taifa gani ambalo ubaguzi unajengwa kwa rangi na
vyama, kama ubaguzi huu utaweza kuondolewa kwa sisi kujiuzulu, nafasi zetu zote
mpaka na mwenyekiti wa taifa, lakini taifa hili likabaki na mshikamano tutafanya
hivyo hata kesho. Undugu ni bora kuliko rangi na vyama vya siasa,” amesema.
