Hizi hapa mechi za nusu fainali Europa League leo Alhamis Mei 3, 2018

Mechi za marudiano michuano ya Europa League zitachezwa usiku wa leo ambapo Arsenal watakuwa  ugenini nchini Hispania kuvaana  na Atletico Madrid.

Timu hizo mbili katika mechi ya kwanza zilitoka  sare ya bao 1-1.

Mchezo mwingine wa leo ni  wenyeji Salzburg ya Austaria watakao pambana vikali dhidi ya  Marseille ya Ufaransa ambayo iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika mchezo wa awali.

Timu mbili zitakazofanikiwa kufuzu baada ya mechi za leo, zitakutana kwenye fainali za michuano hiyo  itakayofanyika Mei 16 nchini Ufaransa.

Post a Comment

Previous Post Next Post