ACT kusaka viongozi wa kitaifa mwezi Agosti ikijiandaa na uchaguzi serikali za mitaa, mkuu


Chama cha Act-Wazalendo kinatarajia kufanya uchaguzi wa viongozi wa kitaifa katika chama hicho ili kuimarisha muundo wake kuelekea maandalizi ya ushiriki wa uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwakani, na uchaguzi mkuu wa 2020.

Taarifa hiyo imetolewa leo Mei 27, 2018 na Katibu wa Itikadi na Uenezi Act, Ado Shaibu wakati akizingumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Ado amesema viongozi wanaotarajiwa kuchaguliwa kwenye uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika jijini Mbeya mwishoni mwa mwezi Agosti mwaka huu, ni kiongozi wa chama, mwenyekiti wa chama taifa, makamu wenyeviti wa bara na Zanzibar na wajumbe wa kamati kuu.

“Tulisema 2018 pamoja na mambo mengine utakuwa mwaka wa kuimarisha muundo wa chama kupitia uchaguzi, zoezi la uchaguzi linaendelea vizuri lipo katika ngazi ya majimbo kwa sasa, na hivi karibuni tutaingia ngazi ya mikoa, uchaguzi wa viongozi ngazi ya kitaifa utafanyika mwishoni mwa agosti kwa kuanzia 25 hadi 27,” amesema Ado na kuongeza.


“Viongozi wanaopaswa kupatikana kupitia uchaguzi, ni kiongozi wa chama, makamu mwenyekiti Zanzibar na bara, wajumbe wa kamati kuu hawa wote wanapatikana kupitia uchaguzi, katiba inasema uchaguzi unatakiwa kufanyika kila baada ya miaka mitano lakini kutokana na sababu mbalimbali utafanyika mwaka huu ikiwa ni miaka mitatu imepita tangu viongozi kuchaguliwa, ili tujiandae chaguzi zijazo.”

Post a Comment

Previous Post Next Post