Diva amshushia matusi Michael Lukindo


Na Abdul Hussein, 24SevenUpdater

Kwa hali isiyo ya kawaida jana mtangazani wa Clouds Fm Diva maarufu kama Divetheabawse amemshushia mvua ya matusi aliyekuwa  mtangazaji mwenzake Michael Lukindo maarufu kama MR Infoma

Lukindo ambaye kwa sasa amejikita kwenye uimbaji wa muziki wa kizazi kipya alijikuta katika wakati mgumu alipo kuwa anatambulisha wimbo wake mpya wa "Basi iwe" wiki iliyopita ndipo alipo ulizwa na mmoja wa watangazaji wa Cloud Fm Mamy Baby juu ya uhusiano wake yeye na Diva

Lukindo hakuweza kuweka wazi moja kwa moja kuhusu  mahusiano yao na mwana Dada huyo bali alibaki kujikanyaga kanganya juu ya swali hilo

Hata hivyo Mwana dada huyo hakuweza kusema chochoti kuhusiana na tuhuma hizo za kutoka kimapenzi na Lukindo

Kupitia kipindi cha XXL  jana kwenye kipengele cha Shilawadu kinachoongozwa na Soudy Brown, Lukindo alikili kutoka kimapenzi na Mwana dada huyo ambapo Soudy aliwaunganisha wawili hao kupitia simu ya  Ndipo Diva alimshushia matusi Lukindo na kudai kuwa atamshitaki kwa kosa la "defamation"(kashifa).



Post a Comment

Previous Post Next Post