Mil. 200 zawaweka kuti kavu mameneja masoko


Mameneja masoko watano kutoka masoko ya Mabibo, Shekilango, Mahakama ya Ndizi, Simu 2000 na Sinza namba mbili, wamekalia kuti kavu baada ya Kamati ya fedha ya Manispaa ya Ubungo kuagiza wasimamishwe kazi.

Kamati hiyo imemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, John Kayombo kuwasimamisha kazi mameneja hao kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za mapato zaidi ya milioni 200.

Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob amesema ubadhirifu huo umegundulika kufuatia ukaguzi wa ndani uliofanywa na mkaguzi wa manispaa hiyo.


Amesema fedha hizo ambazo ni kati ya Sh. Bilioni 1 zilizokusanywa katika kipindi cha miezi tisa hazikupelekwa benki.    

Post a Comment

Previous Post Next Post