Baada ya Bunge kumzuia Waziri Mkuu kujibu sakata la waraka wa KKKT, upinzani wakoleza moto


Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-KKKT na Baraza la Maaskofu Tanzania-TEC yameombwa na kambi rasmi ya upinzani bungeni kutojibu barua waliyopewa na serikali hivi karibuni.

Barua hiyo ya serikali ilitoa maagizo kadhaa ikiwemo ya kuyataka makanisa hayo kufuta waraka wa pasaka ndani ya siku kumi.

Akizungumza na wanahabari bungeni jijini Dodoma leo Juni 7, 2018, Mbunge wa Vunjo, James Mbatia ndiye aliyetoa msimamo wa wabunge wa upinzani ambapo alisema kuanzia sasa watatumia mbinu mbalimbali ndani na nje ya bunge kuitaka serikali kutoa majibu ya kina kuhusu maagizo hayo.

Msimamo huo wa wabunge wa upinzani umekuja baada ya Naibu Spika, DKT. Tulia Ackson kumzuia Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kutojibu swali kuhusu agizo la serikali la kuitaka KKKT kufuta waraka wake ndani ya siku kumi.


Mbatia ndiye aliyeanzishja mjadala huo bungeni katika kipindi cha maswali na majibu aliyetaka kujua ukweli kuhusu barua hizo.

Post a Comment

Previous Post Next Post