Chadema yapata pigo Moshi


Chama cha Chadema kimepata pigo baada ya diwani wa kata ya Mawenzi iliyoko Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Hawa Mushi kufariki dunia jana Juni 7, 2018.

Mushi alifariki dunia jana majira ya jioni akiwa njiani kuelekea Hospitali ya Rufaa ya KCMC baada ya kuzidiwa akitokea hospitali ya St. Joseph.

Taarifa ya kifo hicho imethibitishwa na Mwenyekiti wa Chadema Kilimanjaro, Joseph Selasini.


Selasini amesema mazishi ya marehemu Mushi yatafanyika kesho Juni 9, 2018 nyumbani kwa wazazi wake maeneo ya kata ya Rau.

Post a Comment

Previous Post Next Post