Tochi za barabarani zafanyiwa uhakiki


Kufuatia siku ya vipimo duniani, Wakala wa vipimo wa serikali wanaohusika na kufanya ukaguzi wa vifaa vya biashara, usalama, afya na mazingira (WMA)  wamefanya zoezi la uhakiki wa speed radar (Tochi) za barabarani kama zinafanya kazi vizuri.


Zoezi hilo limefanyika Vigwaza, wilayani Kibaha mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku hiyo.

Mkuu wa Kitengo cha Elimu na Mafunzo wa Kikosi cha Usalama barabarani Tanzania, Abel Swai amesema mara kadhaa wamekuwa wakijitokeza madereva kulalamika kuwa wanakamatwa kwa kutumia tochi hizo kwa spidi ambazo sio za kweli lakini matokeo ya uhakiki wa vipimo hivyo yanaonesha kuwa havina tatizo.
“Hii tuliofanya leo ni kuwaambia wananchi kuwa vifaa hivi vipoje kama wakala wa vipimo wamejiridhisha maana yake ni sahihi hivyo pasitokee mtu akalalamika kuna wakati mwingine wanakamatwa kwa spidi sio za kwao,” amesema Kamanda Swai.
Aidha Mkurugenzi wa Ufundi wa Wakala wa Vipimo wa Serikali, Stella Kawa, amesema tochi zote zilizohakikiwa zote zinapima vizuri.
“Ukiambiwa ni km 80 au km 70 basi ni 70 kweli, tunawaambia watumiaji wa magari kwamba unapohisi una wasiwasi na vifaa hivyo basi wafanye mawasiliano na wakala wa vipimo kwa msaada zaidi.

Post a Comment

Previous Post Next Post