Viingilio vya mechi ya Simba Vs Yanga Mei 29 hivi hapa


Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetaja viingilio vya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu wa 2017/2018 kati ya Simba na Yanga utakaochezwa Mei 29 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Katika mchezo huo namba 178 utakaofanyika Saa 10:00 jioni, kiingilio cha chini kitakuwa shilingi 7,000 wakati kiingilio cha juu kitakuwa shilingi Elfu Thelathini.


Jukwaa la VIP A itakuwa shilingi Elfu Thelathini (30,000),VIP B na C shilingi Elfu Ishirini (20,000) na Upande wa Mzunguko kwenye viti vya rangi ya Chungwa,Bluu na Kijani itakuwa shilingi Elfu Saba (7,000)
Tiketi tayari zimeanza kupatikana kuanzia sasa kupitia Selcom

Post a Comment

Previous Post Next Post